Wednesday, November 28, 2012

MSANII SHARO MILLIONEA AFARIKI DUNIA TANGA


Msanii maarufu wa filamu na Vichekesho nchini almaarufu kama Sharo Millionea amefariki Dunia Kutokana na Ajali ya Gari  alilokuwa akiendesha aina ya Harrier eneo la Muheza Mkoani Tanga.
Kwa mujibu wa mitandao mbalimbali nchini inasema Kamanda wa Polisi mkoani Tanga Constatine Masawe amekiri kutokea kwa msiba wa Sharobaro, baada ya kupata ajali majira ya saa 2 usiku katika kijiji cha Lusanga, Muheza ambapo pia ndio nyumbani kwao.
Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya mkoa wa Tanga.
Msanii huyo maarufu ambaye amefanya tangazo la mtandao wa simu za Mkononi wa Airtel pamoja na Tangazo la Kinywaji cha Azam Cola akishirikiana na mwenzake King Majuto  ambayo yamekuwa kivutio kwa watoto na wakubwa kutoka na staili ya kuweka mdomo pembeni akionyesha jinsi gani mashabaro walivyo.
JIMMY CHUMA BLOG: Iko pamoja na Familia ya marehemu sanjari na Watanzania wote  kwa ujumla katika kuomboleza msiba huu mkubwa wa mpendwa wetu Sharo Millionea.
Mungu ailaze roho ya Marehemu Mahali pema peponi Amen.

Wananchi wakiangalia gari lililosababisha kifo msanii Sharo Milionea
Marehemu Sharo Milionea (kulia) na Marehemu Steven Kanumba enzi za uhai wao.


No comments:

Post a Comment

Unaonaje hii?