Pichani Meli ya LCT Islanders ikiwa imezama Pwani ya Nungwi, Unguja. Picha kwa hisani ya Zanzinet. |
Meli ya LCT SPICE ISALNDERS imebinuka na kuzama katika Bahari ya Hindi huko Pwani ya Nungwi, Mkoa wa Kaskazini Unguja wakati ikielekea
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu wa Zanzibar, Mhe. Haji Issa Ussi akithibitisha tukio hilo amesema kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa nane na nusu usiku wa kuamkia leo ikiwa imebeba abiria 610 pamoja na mizigo.
Mhe. Ussi amesema kuwa meli hiyo iliondoka Bandari ya Malindi Unguja ikiwa katika hali ya uzima kabisa lakini katikati ya safari ikatokea hitilafu na kusababisha kubinuka na hatimaye kuzama. Hadi sasa bado haijafamika idadi kamili ya watu waliofariki katika ajali hiyo lakini vyombo vya uokozi vimefika katika eneo la tukio ili kutoa msaada.
Serikali imewaomba wanananchi kuwa watulivu na taarifa zaidi zitakuwa zikitolewa kuhusiana na ajali hiyo kwa ujumla.
No comments:
Post a Comment
Unaonaje hii?